Powered By Blogger

Tuesday 23 February 2010

YA VVU PEMBA NA MAJUMBA YA DHAHABU


Na  Ally  Mbarouk

Pemba Peremba!
Pengine   kwa  wakaazi  wa Zanzibar  mengi tumeshayasikia  kuhusa  mji  unaoitwa   Miembeni  .Hapa zizungumzii miembeni  ya Pemba   banda taka , aaah   ,  wala  sizungumzii Miembeni ya  Mkoani , ni   Miembeni  ya 
Unguja  ;mkabala  na 


Michenzani  ...nyote  mnapajua . Basi  kama umeshasikia  na umeshapajua  hebu panda boti . Sikupandishi  Serengeti ukalala baharini   nakupandisha   ndege  mpya   ya Air  Zahra  au sijui  Zara..ufike  mara  moja . Ukifika uwanja wa ndege  chukua tax  hadi  Machomane .Ama kama miji ingalipewa   majina  kulingana  na tabia za mitaa  hii ningaliita    Miembeni ya Pemba .

Nisikuzungushe :  mara  amba Serengeti , mara Air   Zara   mara  Machomane   , hebu tuende  katika wazo nililolifikiria katika  makala  haya . Pengine     nimenasibisha   mitaa  ya Miembeni  na    Machomane  Pemba kwa  vitabia na vijitabia  fulani  fulani hivi  vya mitaa  .  Si  unayakumbuka mambo yetu    yalee  tuliyozoea;yanayowafanya    vijana  kutoka  mate, kuwa machizi taahira .Mambo yale   yanayowafanya  vijana  kukosa  dira ya maisha   na na kuwa   mazoba  , ombaomba na  vibaka  wakubwa mitaani .Mambo ya enzi zile na za  sasa    yanayowafanya  vijana kuishia jela  kwa makosa  ya  wizi , ubakaji    na  mengine .Si kwambii  ni mambo gani wewe mwenyewe  umeshayajua.  Mambo tuliyoyaundia tume na  vikosi kadhaa  vya kupambana  nayo ...lakini  wapemba  wasema  , nkuchukua maji kwenye fuu tomo   ama  maji kwenye  pakacha . 

Nimeanza  kwa kicha  cha  habari  "Jumba la  Dhahabu".Najua hapa fikra  zako zitaanza kukupeleka kwa  Jini Kabula  ,Kojac  , Mzee Chilo na wengine ;wasanii waliobobea  katika  fani ya maigizo ya  luninga .  Mi  siko  huko   akhui,  usiwe na  haraka za chura   ,,,ukaruka  ukangia   mumo!

Kwa mitaa ya  Machomane ukizungumza upelekwe  Jumba la Dhahabu  , hee  watu  watakushangaa  .Kama  una  joho na  kilemba watakwamia  , ssalaleee  mjomba  hata   weye ? Lakini  Wapemba wana  msemo wao  maarufu  , "Nkongwe  haina   shehe!"  
Ndio hivyo majumba ya dhahabu yapo yamejaaa .Si Machomane tu mtaa nilioufananisha na Miembeni ya Unguja lakini hata Msingini , Kichungwani , Wawi majumba hayo yapo .Wapemba wasema n’dezo biashara ni mapatano.

Ndio wamehamia na majumba wamekodishwa na wazawa ambao wanasifika kwa kuswali na manundu ya sijida .Wengine wanasema ni watu kutoka ‘waja leo , warudi leo kule kunakotajwa ndio makao makuu ya mahaba dunia ;Simba anakongolewa sharubu na akapigishwa msuaki.Wenyewe ukiwauliza wanasema wamekuja kutafuta maisha kwani Zanzibar biashara ipo wanunuzi wa kumwaga . Wanajitahidi kutangaza mitaani , kwani waswahili wanasema biashara itangazwayo ndio itokayo .Hawana mazoea ama kutunza utamaduni wa Kizanzibar wa kufaa matandio , maninja na mashungi , wala .Wanavaa za kisasa na wapitapo mitaani huambiwa , Muungano udumuuu! Na ni kweli muungano unadumishwa na faida ya muungano inaonekana .

Biashara inaenda kwani wenyewe wanasifu kwamba kutokana na vigenzo vya kumlinda mlaji bidhaa inauzika .Na kwa nini wasiuze walaji wapo .Kwani unadhani wanakula watu wa mbali ; ndio hao hao bin kinaanata bin huzaimata bin ilyasa.Wenye wake zao waliotulia majumbani .Au vijana wadogo wa shule ambao ndio kwanza hawajajua utamu wa pilau , wameujulia kwao!

Sisemi maneno haya kwamba labda miongoni mwa wauzaji na wenye mji hawamo .La hasha wapo tele . Wengine ndio hao hao baadhi yao wanaovaaa tarabizuna na ninja ili wanapokatisha mitaani wasionekane . Na wala sithubutu kusema kwamba kila waliotoka huko na kuja kupanga kwamba wanafanya hivyo , la hasha .Wapo waungwana na heshima zao .Wamekuja kutafuta maisha.Wanajituma na kutafuta riziki kwa bidii. Wameanzisaha biashara zao na maisha yanakwenda .Wamewaacha wenyeji wakikaa barazani na kuzungumza mambo ya harusi.Kupigana michango ya kila siku ya machai ya harusi na maholi ya rusha roho.Kwao si shida kukipata kila kitambaa au fasheni ya baibui inayoingia mtaani . Wana wasiwasi gani na allah riziki analeta

Nakumbuka siku moja nilikua na kajiutafiti kidogo pamoja na wenzangu .Miongoni mwa tuliozungumza nao ndio hao hao kamata mkia chinja . Mmoja alipoulizwa kwa wiki unaweza kuuza bidhaa kwa watu wangapi alisema , “ Naweza kupata watu 10 , saba hadi sita’’. Kwa bei ya shilingi ngapi akasema .Ndio hivyo hivyo tu, wengine wanakula baadae hawalipi , lakini sh elfu saba nane hadi tano” . Alipoulizwa tena kama umekosa mteja huna pesa unafanya nini”” Basi alijibu unajua wengine ni maarufu hapa .Tunabadilisha bidhaa kwa bidhaa ….kama kilo tatu za mchele , lakini ukikosa unakwenda hata kwa 2000.Unadhani tutafanyaje na maisha magumu” Alisema

Haya kama bidhaa imefikia kuuzwa kwa shilingi 2000 unadhani nani atashindwa kununua .Unajua wazee wengine pesa kama hiyo anampa kijana wake atumie shule kila siku .Ndio yaliyomkuta kijana mmoja ambae sitomtaja jina .Alikua akipewa pesa za kutumia skuli anakusanya na zinapotimia elfu 4000 tu anakimbilia majumba ya dhahabu .Hakujuilikana na na wazazi wake hadi alipopata maradhi ya kuambikiza (kaswende) .Siri ikatoboka kwani alipobanwa na wazazi wake alitoa ushuhua pamoja na kuwataja marafiki zake wote wenye mchezo kama huo .

Naandika nukuu hii nikiwa na wasiwasi sana kwamba huko twendako na vizazi vyetu siko .Sikatai kufaidi matunda ya muungano wala siipingi kauli ya kwamba Zanzibar ni njema na atakae aje, bali nakihofia hichi kizazi na haya maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI

.Zanzibar ni ndogo sana.Mitaaa ina watu kidogo sana .Kama itakuepo tabia ya kubadilishana bidhaa basi sijui khatima yake nini

 

Pale mwanzo tulikariri kauli mbiu ya mapambano dhidi ya UKIMIWI yaani A-Acha kabisa, B-Be Faithfull yaani kuwa muaminifu na mkeo, nay a tatu C - Use Condom .

Du hii C inaleta mijadala kila unapoitaja .Lakini kinachoonekana kwa sasa A inaanza kushindwa nguvu , B ni ya wachache waliookoka , na C haipatikani hata inapohitaji na maadili hayaruhusu kutumia . Hapo ndipo penye kitendawili cha Tembo kutengwa kwa ubambe kwani wenye bidhaa wanasema , chakula ni cha hoteli mlaji ana hiari yake .Kula kwa kijiko ama mkono mtupu . Lakini kwa kauli yao mmoja alisema wengi wa wateja hawapendi kula kwa kijiko, eti wanakosa ladha.Wanalazimisha mkono mtupu na wanapofanya hivyo bei ya chakula huongezewa na huridhia kama kuku anaetaga .

Nakumbuka zamani nilipokuwa nafunzwa masuala ya kuchochea mabadiliko ya tabia niliambiwa kwamba kuna mikabala mengi ya kufanywa na jamii kama jamii imedhamiria kuondosha maovu .Mkabala mmoja nitakuhadithia .Kama ni mkaazi wa Unguja bila shaka umeusikia ujasiri wa watu wa miembeni waliposema vilabu vya pombe chini ya mapaa ya nyumba zao basi.Walinyanyua sauti.Wakatishia kuchukua hatua mikononi mwao iwapo serikali itashindwa .Waliamua hivyo kwa sababu waliona kuwepo kwa vilabu hivyo ni tatizo kwao na familia zao.Pombe ziliuzwa kama maji ya kunywa .Wanouza miili yao wakaona ndio sehemu pia ya kujipatia wateja .Baraza za majumba yao zikawa ndio magodoro ya kufanyia ngono giza liingiapo.Magamba ya kondom yakazagaa kila chochoro ya mtaa .Majumba ya dhahabu yakawepo kila kona na watoto wakajifundisha kula bata bila manyoya .

Basi wakaazi hao wakaona uchungu.Serikali baadae ikachukua hatua kwa kuziondoa baa hizo.Hivi karibuni nimesikia kuna mikakati ya kuyaondoa majumba ya dhahabu .Toba sikio , nasikia hivi karibuni nyumba moja iliungua moto sambamba na baa maarufu Jonzani .Haya wa Miembeni lakini kama hili linawachoma mbona madawa ya kulevya yanauzwa mchana na mumetulia .Vijana wanaangamia ?
Nisiseme sana kama nimemeza vocha ya dola 50.Nilichokusudia kusema Pemba ni ndogo sana .Mzunguko wa watu ni wa wale wale.Iwapo maambukizi ya UKIMWI yatakuwepo kwa makundi Fulani ya watu basi watu hao hao huwa na muungano mkubwa na jamii yote kiasi ambacho ni mwanya kwa virusi kusambaa hata kwa yule alietulia nyumbani akimsubiri bwana alete mapembe .

 

Bado kazi ipo ya kupambana na matatizo haya nikiitupia jukumu jamii yenyewe kuwa chanzo cha mabadiliko.Majumba ya dhahabu yapo na yanaendelea kuwepo lakini bado tunaweza kutumia mikabala ya jamii kwa njia za ustaarabu na kubadilisha hali hii .

JASIRI HATUNAE TENA

NA   ALLY   MBAROUK OMAR
BWANA SALUM ALI SALUM


ZANZIBAR YAPOTEZA SILAHA YA MAPAMBANO YA UKIMWI


SHUHUDA JASIRI ,JEMEDARI HATUNAE TENA

Marehemu  Bwana Salum  Ali  Salum   akifungua moja kati ya  vikao  vya kupambana na UKIMWI


Ya rabi mola mananiiiii ……..oooooooooh
Utupe Kinga na tiba
Ugonjwa huu jamaniiii……..aaaaah
Usiwe kwetu msiba
Vijana wavitandaniiiii ……….aaaaah
Wao pamoja na baba…ooooh
Sote tuko mashakani ……….eeeeeeh
Ukimwi jama ukimwi ……..iiiiiih
Mola tupe , kinga na tiba .

    Pengine umeshawahi kuusikia wimbo huu ; ukiimbwa kwa sauti nzuri inayoweza kumtoa nyoka pangoni. Basi kama hujausikia pengine uliwahi kuhudhuria katika maadhimisho ya kitaifa ya siku ya Ukimwi duniani mwaka 2008 hapo katika uwanja wa Gombani ambapo mgeni rasmi alikua ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr. Amani Karume .



Basi sauti hii ni ya jasiri, shuhuda aliyejitolea katika mapambano dhidi ya Ukimwi marehemu Salum Ali Salum au maarufu , Bwana Salum au sisi tuliomzoea tulikua tunamwita tu Samandalo yaani Babu lao .
Alikua mcheshi mpole aliejaaa hekima na busara .Alimheshimu kila mtu mdogo kwa mkubwa .Unapokaa na bwana Salum utakata mbavu tu, maneno yake ni matamu kama asali au unaweza kumwita ‘kidomo sukari’.Alipokua hospitali Muhimbili kabla ya kuenda Tanga ambako mauti yalimchukua nakumbuka tulikua tunazungumza mara kwa mara .Daima sauti yake ni ya busara na mtulivu sana .Nakumbuka siku moja baada ya kumjulia hali aliniuliza . “Mapambano yanaendeleaje huko?”.Daima alitoa ushauri nini tufanye pale penye matatizo na changamoto”
Kama kujishughulisha na mapambano dhidi ya Ukimwi unatunukiwa nishani za jeshi na mimi nikawa ndio amiri jeshi mkuu basi bwana Salum Ali ningempa nishani ya juu ya utumishi wa jeshi yaani Field Masher ikiwa hichi ndio cheo cha juu. Nasema hivi kwa sababu alikua mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya Ukimwi hapa kisiwani Pemba au Zanzibar kwa jumla .
Nakumbuka enzi zile hapa kisiwani Pemba ambapo anaeishi na virusi vinavyosababisha UKIMWI alionekana ni kama balaa; watu wakasutwa , wakasemwa kwa maneno mabaya na kutengwa katika jamii .Basi yeye kwa ujasiri wake akawa mtu wa mwanzo kujitokeza hadharani kwa Pemba na kuzungumzia hali yake .Hakuona aibu ya kuzungumza na vyombo vya habari kwa uwazi na ufasaha .Akawaelimisha wengine na kuwapa faraja .Akawa kimbilio la ushauri kwa watu waliopatwa na tatizo kama lake .Alijitolea muda wote katika mapambano na kamwe hakua mbabaishaji wala mwenye tamaa .
Nakumbuka siku moja tukiwa katika uhamasishaji huko Kangani pale aliposema “ Watu hawaniamini nikisema kwamba naishi na virusi.Wanasema nimepewa pesa na Serikali ili nielimishe Ukimwi.Wanasema bwana Salum wewe muongooo , mtu mwenye Ukimwi atakaa hivyo? Basi niwaambie Ukimwi upo na hapa Kangani upo na mimi naishi na virusi.Kama hamuamini kadi yangu ya dawa hii” Maskini akaitoa kadi yake ya kuchukulia dawa za ARV hadharani , watu wakamshangilia kwa ujasiri wake .
Ndivyo alivyokua Bwana Salum ambae alikua na ari na nia ya kweli ya kuwaelimisha wengine.Ujasiri na uimara wake ulikua mkubwa mno kwani kwa kujitolea alianza kuwatafuta na kuwashauri watu wenye hali kama yake ili wawe na sauti moja na vilio vyao visikike ;visiwe vilio vya samaki machozi kwenye maji .
Dk Juma Massoud wa WAMATA Pemba alisema . “ Kwa kweli ilikua ni kazi ngumu ya kuwakusanya watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi pamoja ,lakini yeye alitusaidia na bila msaada wake tungalikwama”.Alisema na kutanabahisha kwamba WAMATA wametoa mchango mkubwa kusaidia
Waswahili wanasema papo kwa papo kamba hukata jiwe na umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu.Ndio kazi aliyofanya bwana Salum ya kuwaunganishwa watu pamoja hadi hapo ilipozaliwa rasmi Jumuia ya Watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi Pemba ,ZAPHA+.Hii ilikua ni kwa ajili ya kuunga nguvu jumuia hiyo ambayo makao makuu yapo Unguja . Na mara tu ilipoundwa na wanachama kukaa pamoja juhudi zilifanywa za kutafuta uongozi .Ninakumbuka siku ya uchaguzi uliofanyika Ukumbi wa TC chachani .Unadhani kulikua na mgombea mwenza .Unadhani alipiga kampeni ….wala ! Wanachama walimchagua kwa ushindi wa kishindo kama si wa sunami! Alishajitangaza .Hakua na mpizani .Unadhani nani angejitokeza , labda angepata hiyo kura yake tu!
Hayo alifanya kwa nia ya dhati hadi hivi leo wanajumuia wanatambulika kwa kazi yao nzuri wanayofanya .Wamesaidaia sana harakati za mapambano hasa katika kupunguza unyanyapaa .Hivi leo nani asietambua mchango wa ZAPHA+ ambapo kwa ujasiri wao wamejitokeza na kufungua matawi kila wilaya hapa kisiwani Pemba kiasi cha kufikia wanachama 235 kwa sasa .Hii ni hatua kubwa kwani hapo awali aliejitokeza alikua ni jemedari huyu tunaemzungumzia .
Leo ZAPHA+ kwa juhudi zake na wengine imesimama.Wanachama wamejikusanya pamoja na kufanya mambo mengi ya kutoa elimu na miradi midodo midogo ya maendeleo
Ndivyo alivyokua .Alikua mtu wa watu ,anaependwa na kila mtu .Labda nisimwagie sifa peke yangu.Nilipozungumza na mwenyekiti wa Zapha+ , Consolata John mara baada ya msiba huu , mwanzo alisema .



“Hili ni pengo kubwa si kwa Zapha+ Pemba tu bali kwa Zanzibar nzima” Ndivyo alivyomuelezea marehemu bwana Salum na kuongeza , “Alikua mchapa kazi asiechoka .Alietumia muda wake mwingi kujitolea kwa hali na mali kwa kazi za jumuia .Alikua ni kiungo muhimu .Kweli tumeondokewa na mchapa kazi hodari” Alisema Consolata kwa huzuni
Nikizungumza na mmoja wa wataalamu anaefanya kazi kwa karibu na ZAPHA+ , Seif Juma alizungmza mengi yanayomuhusu Bwana Salum.Alisema si kwamba hakua mtu alieshika nafasi za uongozi hapa Zanzibar tu bali hata ndani ya Afrika ya Mashariki . “Alikua ni mjumbe wa Bodi ya Mtandao wa watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi wa Afrika Mashariki pia akiwa kama ni mweka hazina wa jumuia hiyo .Hii kwetu ni heshima kubwa kwa mzanzibari kushika wadhifa kama huo” Alisema Seif na kuongeza kwamba ,Bwana Salum alikua mtu muelewa wa mambo mengi na aliisaidia sana jumuia .



Nae mratibu wa Tume ya Ukimwi Pemba , Nassor Ali Abdalla alimtaja Bwana Salum kama kiungo muhimu sana cha mafanikio, . ‘’Hapa tumepoteza mtu , alikua ni kiungo muhimu kati ya Tume ya Ukimwi ,ZAPHA+ na jumuia nyengine”.
Pengine bwana Salum aliona kwamba pamoja na kuwepo ZAPHA+ bado juhudi zilihitajika za kuanzisha jumuia nyengine za maendeleo na mapambano ya UKIMWI .Mnamo mwaka 2007 alikua mwanachama muanzilishi wa jumuia ya JUKUVUM ( Jumuia ya Kupambana na Virusi vya Ukimwi Mkoani ) .Jumuai hii kwa sasa inaendelea na miradi mingi ya mapambano ya UKIMWI.Pamoja na nafasi hii pia alikua ni mjumbe wa Kamati ya Wilaya ya UKIMWI nafasi ambayo ameitumikia kwa mafanikio makubwa .
Mara tu baada ya kutokea msiba wa kifo chake ,mtaa wa Mkoani Mapinduzi ulikua kimya .Anasimulia Moh’d Rashid mkaazi wa hapo .


“Kama siamini hivi, naona kama tutapishana njiani sasa hivi.Yaani siamini” Alisimulia .


Hivyo ndivyo alivyokua .Nyumba yake alipokua anaishi ilipachikwa kila majina .Wengine waliita Angaza.Hii ni kwa sababu pia alitumia kama sehemu ya kuwapa watu ushauri nasaha kwa anaepata tatizo kama hilo .Alihudumia wagonjwa , kuwapa faraja na misaada ya hali na mali .Aliwafata popote walipo tena kwa kutumia nauli yake si ya jumuia pale lilipotokea tatizo . Kazi hii aliifanya kwa nia safi, bila malipo wala ushuru wowote akishirikiana na mke wake mpendwa , Bi Aisha Rashid


Familia yake yote kwa hapa Pemba ameihamasisha vizuri .Watoto wake akina Fatma na Zahra ni waelimishaji wazuri katika jamii.Kwa kupitia klabu ya watoto au ToTO KLABU wameanzisha kikundi cha uhamasishaji na siku zote huwamwaga watu machozi katika mahafali mbalimbali za kuelimisha jamii kwa kutoa ujumbe wenye hisia kali .


Mke wake mpenzi Bi Aisha Rashid pamoja na kazi kubwa anayofanya ya uhamasishaji pia ni mshauri nasaha katika kituo cha MCT na CTC Mkoani na anafanya kazi hiyo kwa mafanikio makubwa .Yeye mwenyewe anajulikana kwa jina la “MAMA USHAURI”
Kama kuma kuna mtu anahitaji kupewa sifa kubwa kwa kupambana na vitendo vya kuwadhalilisha na kuwatenga watu wanaoishi na virusi vinavyosababisha UKIMWI kwa Pemba basi Bwana Salum ni namba moja . Ni yeye alietilia mkazo kuanzishwa kwa kampeni hii na kuwashawishi wengine wajitoe kupambana na unyanyapaa. Basi wana ZAPHA+ wakaungana na kampeni hii kwa nia ya dhati hasa kwa kutoa ushuhuda . Kwenye mikutano ya hadhara, semina na warsha , kwenye majimbo na shehia kote wakafika huko kuelimisha wananchi . Jasiri huyu akawa mstari wa mbele kuhamasisha hadi hii leo mipapai iliyochumwa na mtu mwenye VVU haikatwi tena na maandazi barabarani yananunuliwa . Leo hii ninapoandika makala hii ZAPHA+ si tatizo katika jamii bali ni suluhisho la kukimbiliwa na wengi.
Kwa ujasiri huu na kushirikiana na taasisi kama vile ZAC , WAMATA , USAID , CLINTON FOUNDATION ,ZACP , CVM wana Zapha wakajitoa . Sasa wanatumika kutoa ushauri nasaha katika hospitali kubwa, kutoa na kusaidia huduma majumbani pamoja na kujikusanya pamoja na kuanzisha miradi ya maendeleo . Kama si juhudi za kamanda huyu aliekua na kipaji kikubwa cha kuunganisha watu , yote haya yasingefikiwa .
Maisha ya familia ya bwana Salum ni ya furaha yaliyojaaa matumaini. Wote ni wana mapambano dhidi ya Ukimwi.Muambata wake mkuu ambae ni mke wake kipenzi , hadi Bwana Salum anaaga dunia , nae ni jasiri mwenye uthubutu katika mapambano.Wote kwa pamoja walijitoa hadharani na kuelimisha jamii .Si jambo la kushangaza kupanda jukwaani pamoja na kuelimisha kuhusu Ukimwi.Siku moja tukiwa katika kampeni ya kupambana na unyanyapaa kwa Wilaya ya Mkoani nakumbuka walisimama pamoja na kuimba wimbo huu.
Twende wapi twende wapie eee mama eee mama
Tumueleze nani matatizo yote sisi wana Zapha @2
Mitaani wanatukataa
Majumbani wanatunyapaaa
Ee mola tusaidie
Tuna kilio eeeh
Tuna kilio eeeeeh …..mama
Twende wapi , twende wapi ooooooh mama @2
Tumueleza nani matatizo yetu yeeetu , sisi yatima
Tumueleze nani matatizo yetu , sisi kama yatima
Wakiimba wimbo huu kwa hisia kali na vibwagizo , watu walibubujikwa na machozi .Nakumbuka alikuwepo Naibu Katibu mkuu , Mhe Msham Abdalla Khamis ambae ni rafiki mkubwa wa Bwana Salum. Katika hotuba yake aliyoitoa mkutanoni hapo , Mhe Msham hakuacha kumwagia sifa jemedari huyu wa mapambono kwa kumtaja kwamba ni mtu wa aina yake mwenye kila sababa ya kupongweza kwa jukumu zake za kuelimisha jamii. Nikuhadithie kitu , kwa ushawishi wa Bwana Salum na ari ya Mhe .Msham ya kuungana na jumuia hiyo alichukua uanachama wa jumuia ya ZAPHA+ akiwa ni mtu kama wa pili aliejiunga na jumuia hiyo pasi na kuwa anaishi na virusi.Katiba ya jumuia ya ya ZAPHA+ inaruhusu kwa watu wengine kujiunga na jumuia hata kama huishi na virusi vinavyosababisha UKIMWI .
Kwa wakaazi wa mjini Tanga handeni takriban miaka kama 35 iliyopita jina la Salum Ali Salum lilikua maarufu sana.Alisifika kwa sauti yake nyororo na manjonjo apandapo jukwaani akiwa na kikundi cha taarab .Nakumbuka siku moja enzi za uhai wake alinihadithia

“Aaaa bwana Ali , enzi hizo Salum nikiwa Salum nilikua natisha kwenye taarab” Alisema hapo akaniimbia kipande cha mashairi ambacho leo sikikumbuki tena na baadae akacheka sana na akaniuliza . “Niambie , hapo vipi”. Sikuwa na jipya ni zaidi ya kumkubali tu na kugonga kiganjani kwake . Unajua bwana Salum alikua anapenda kujichanganya na alikubalika na watu wa umri wote .Akikaa na wazee atakua kama wao , lakini akikaa na vijana kama sisi , aaah tulipiga stori hadi basi huku tukikata mbavu kwa utani na mizaha yake .
Ni nani angalikubali kama utamkuta Bwana Salum na kaunda suti zake , kiatu kikali mguuni na bashasa zake na akakueleza kwamba ana miaka 68 akizaliwa mwaka 1942 !Kamwe utabishana nae tu .Alikua anajipenda sana na siku zote alikua smart ,msafi na mtanashati.

Pamoja na wasifu wake mkubwa wa kuitumikia jamii , pia Bwana Salum alikua mtaalamu .Aliwahi kufanya kazi pia na General tyre huko Arusha kama muhandisi
Mwaka 1999 alihamia kisiwani Pemba na alipofika tu aliendelea na kazi yake ya ufundi mifereji kama kibarua chake binafsi .Alikua fundi muadilifu na umahiri wake wa kufanya kazi hii ulimuongezea sifa na kuwafanyia watu wengi kazi hiyo . Kwa maeneo ya mkoani alijulikana pia kama fundi Salum
Jina la Samandalo kwa nyumbani kwao kijiji cha Nandiamba Wilayani Handeni-Tanga lina maana ya “babu yao” ,lakini mwenyewe enzi ya uhai wake alilikuza na kuliita “babu lao”.Ndio hivyo kwani hadi anafariki dunia usiku wa tarehe 15/ 2/2010 kijijini kwao Tanga , akiwa na umri wa miaka 68,aliacha watoto 17 , mjane mmoja na wajukuu 25 .Bila shaka jina la Samandalo au babu lao liliendana na barka yake ya kizazi na wajukuu wengi aliobarikiwa .Nilipomuuliza mke wake ,Bi Asha Rashid unadhani bwana Salum kaacha vitukuu vingapi nakumbuka aliniambia , “Ah! Hilo ni suala gumu kwani inabidi niwapigie wajukuu zake wote walionza kuzaa na wengine namba zao za simu sina!” Alisema na nilimwambia basi kwani haya uliyonieleza yanatosha
  Marehemu Bwana  Salum  Ali   Salum (katikakati)  akifungua  kikao cha TAC  Pemba


Waswahili wanasema pang’okapo jino hukaa pengo na ni kweli .Kwa kuondokewa na shuhuda jasiri huyu pengo gego aliloliacha kamwe haliwezi kuzibika . Ni taa iliyozimika ambayo muangaza wake uliwafikia wengi .Alileta matumaini pale wenzake walipokata tamaa.Akawatia moyo na ujasiri wa kuwaokoa wengine .Hakuwa na kiburi na dharau .Alichapa kazi bila kuchoka kama analipwa madola ya shilingi.
Nakumbuka mengi aliyoyaanzisha .ZAPHA+ Pemba imezaliwa na inatambaa .Badi inahitaji mbeleko za jasiri huyu.Walezi wengine wapo na wanajituma lakini hii ilikua nguzo iliyosimama vyema.


Tumalizie kwa tauhidi ;aandikali mola halifutiki na kalamu ya mola haina makosa .Mungu amlaze mahala pema peponi .AAAMIN RABI AAMINA

Friday 12 February 2010

From journalist to International Space Centre

Its    like    my    birth day . I  open up my    eyes  and look up on  sky. My    mother  came   up and  give  me  a laptop .She said to me  this  is   your  tool  of searching  the   life.I  asked   her   what  can I  suppose  to  do  with this   laptop.Then  she   told    me  open   the  Blogs .
Yes ,ending   up  Zanzibar    internet  journalism ending   love  affairs  .  Thats   you  can    see  the   new word   of  bogs  from  Zanzibar

uzalendo kwanza


Uzalendo kwanza

Thursday 11 February 2010

From Zanzibar to Worlds Legend


Zanzibaris mainly used to call there son as like Ali , Moh’d, Said and many other like to symbolize there long standing traditions of surnames. This is mainly because of long cultural norms of Islamic named inherited from historical Arab colonial rule .



When Mr Peik Johansson mentioned the name of Freddie Mercury as the one the most top rock and roll music legend with originality from Zanzibar , many of the internet journalism training participants swings there heads like a fans to claims that’s may be that was not among the common traditional names of Zanzibar

Yes he is . He was born in Zanzibar in 1946 with the same common names Farouk Bulsara like any other Zanzibaris and live in the one the most long standing old city of Zanzibar known as stone town playing in a narrow street . His family immigrated in Zanzibar from India and his fathers worked for British Government as an accountant .
Back in 1970 , he joined boarding school in India and letter on he moved to London for further studies .

Like a new leaf bad , he was found earlier as music lover playing a piano just as a pleasure with friend but his unique beautiful and powerful voice convinced him to establish a Queen band with his three friends

May be you can not compare Mercury with Michel Jackson based on many thing but one of his best music legend tag was powerful vocals and flamboyant performances although he was a very shy guy in backstage .

Freddie was best known as Britain’s first Asian rocks star and the Times Asia named him as the one most influential Asian heroes on the past 60 years and ranked as an 18 of the 100 greatest singers of all time selling 3000 million copies album

For football lovers in international performances may be you have already hear the high vocal voice of the song “ We are the Champion” as the one of popular songs during football victory . This one among the best ever Freddie powerful song which entitles other popular song like Bohemian Rhapsody, Killer Queen . Crazy Little Thing called Love , Barcelona and many other popular song which picked up high rank in world music charts



 
Life is a like candle in a strong wind or is like an old leaf in tree . That’s during early 90’s there was rumors that ,Freddie was badly ill suffers from HIV/AIDS infections . This rumors confirmed by him that he was conceded by the virus on his public announcement . Mercury die on 24th November, 1991 after severe illness


In Zanzibar my be the Freddie Mercury legendary history is paved because by his personal life style and less aborigine family affiliation background but in the world of music he remain a guru rock on roll music vocalist with excellent skills in stage performances

                                                                                                             Freddie  Mercury

Wednesday 10 February 2010

Wangar Maathai, Lulu ya Afrika



Bi Wangari Maathai
Unaweza kuanza kitu kama utani tu lakini kikawa na mafanikio makubwa sana dunia . Tunakumbuka kuanzishwa kampuni kama microsoft ama TOYOTA ambayo ilikua kama karakana ya familia tu.Leo hii ni makampuni makubwa sana duniani yanayiongiza mabilioni ya shilingi kila mwaka .

Basi ndio hivyo ilivyoanza taasisi ya Wanaharakati wa Mapinduzi ya Kijani huko Kenya ama , Green Belt Movement . Hivi leo kweli utaamini kwamba asasi hiyo iliyoanzishwa na mwanamama jasiri wa huko Kenya . Bi Wangari Maathai , imebeba umaarufu mkubwa sana duniani na hata kufungua ofisi nje ya Kenya kama vile nchi za Ulaya .

Hebu angalia viunganishi vya makala hii fupi uone jinsi mwanamazingiza huyu alivyopania kuleta mabadiliko

Ukiangalia wasifu wa mama huyu bila shaka utakubali kwamba ni mmoja kati ya wanamama shupavu si Afrika tu bali dunia nzima . Amechangia kwa kiasi kikubwa masuala ya kuendleza shughuli za mazingira duniani akiwa mwana falsafa katika tasnia hiyo . Wasifu wake unaeleza kwamba pamoja na kushika nyadhifa mbalimbali huko nchini Kenya pia amefanya juhudi kubwa kiasi cha kutunukiwa tunzo sisizopungua 15 za kimataifa

Tuesday 9 February 2010

What we learnt from yesterday

Yesterday is a one among my favourite day in the world of journalism and internate. It was about opening a big cyber café if not a Burji Khalifa, the world tallest building in Abudhabi .

After a brief introduction from MISA Tanzania about the content of the five days comprehensive training on journalism and internet cybercafé , Mr Peik Johansson our course facilitator introduce to us about him self as a professional journalist and the Finish Foundation for media , Communication and Development as an international media outlet for communication development .
The self introduction was one among the interesting part in which every participate introduce his/ her journalism experience and familiarities with internet to deal with daily journalistic carrier .

Among the topic and subjects introduced was:-
 Internet as a source ;for information , communication, publication , research, shopping , global diary, library, funs and friends , facts findings , banking , booking , entertainment , wikipedia and cyclopedia etc
 How internet has change the society
 Leaning by doing: searching for buying e-ticket from Helsink to Turku ;changing schedule and accurate depart time table
 Web searching and editing : editing Wete population profile and Communication and Media in Zanzibar
 Google map: Searching for Google map and images
 Blogs: opening individual blogspots based on blog address , title and posting
 Top websites and search engines : Google , ebay, amazon ,myspace , you tube , yahoo, Slashdot etc

DAY 2: 9TH FEB, 2010
1 . BLOGGING:
 Viewing individual blogs
 Posting and editing
 Changing layout , setting and templates designing

2 INTERNET WORLD STATISTICS
 Popular world surfing
 Africa internet surfing statistics
 Discussion : factors contributing to

3. POPULAR JOURNALISTIC SEARCH WEBSITES
 Local and international websites
 Tanzania online newspaper : eg ipp media , global publishers
 Tanzania national websites and other links

Its just a two days ending with a three days in hand but honestly i can say that this internate courses has open up my mind to upgrade my journalism carrier . I came to realize that a gentle man from Finland has an experince of opening the doors of internate cyber world

Monday 8 February 2010

JIKINGE


Kumbe twaweza. pakiwa na nia na kusaidiana .
Najua kila mtu anaweza kutoa mchango wake juu ya kupambana na Ukimwi.Tumezoea tu , tunapotaja Ukimwi kwanza tunafikiri pesa kwamba labda inahitaji mabilioni ya shilingi kupambana na ugonjwa huu tena yatoke kwa wafadhili ambao nao wamekubwa na mtikisiko kama si tetemeko la uchumi
Ndio tunaweza kupambana nao kwa kutumia pia rasilimali tulizonazo. Hivi mzee nyumbani kama atakaa na watoto wake na kuwafundisha maadili mema si amechangia kupambana na Ukimwi . Pia kwa wanandoa kama watakaa pamoja na kufundishana maadili ya ndoa kwa kuwa waaminifu katika ndoa zao ili siku moja virusi vya Ukimwi visijipenyeze katika familia vipi si watakua wamepambana na Ukimwi .
Basi mkabala wa waraka huu utajikita zaidi ni kwa jinsi gani tunaweza kupambana na ugonjwa wa Ukimwi kwa kutafuta suluhisho ambazo ziko ndani ya uwezo wetu

Tusaidiane